Khamenei akataa pendekezo la nyuklia la Marekani
4 Juni 2025Matangazo
Kwenye hotuba yake, Khamenei amesema kuwa suala la kurutubisha madini ya urani limekuwa suala nyeti la mazungumzo kati ya Marekani na Iran na kwamba urutubishaji wa madini ya urani linabaki kuwa suala muhimu kwa mpango wa nyuklia wa nchi hiyo.
Iran haitokubali kuzuiwa kuendesha mradi wake wa nyuklia kwa matumizi ya kiraia
Pendekezo la Marekani kuhusu makubaliano mapya ya nyuklia liliwasilishwa kwa Iran siku ya Jumamosi na Oman, ambayo imekuwa mpatanishi katika mazungumzo kati ya waziri wa mambo ya nje wa Iran, Abbas Araqchi, na mjumbe wa Rais Donald Trump kwa Mashariki ya Kati, Steve Witkoff.