MigogoroYemen
Karibu watu 68 wauawa katika shambulizi la Marekani, Yemen
28 Aprili 2025Matangazo
Kundi la waasi wa Houthi wa nchini humo limearifu hii leo na kuongeza kuwa kombora moja halikuripuka baada ya kuanguka kwenye eneo lilikolengwa na timu maalumu inalishughulikia kwa tahadhari kubwa.
Kituo cha televisheni chenye ushirikiano na Houthi cha Al-Masirah kimeripoti kuwa vikosi vya uokozi na dharura vinakabiliwa na changamoto kubwa kutokana na uharibifu mkubwa uliosababishwa na shambulizi hilo la Marekani.
Kulingana na wizara zinazodhibitiwa na Houthi, wahamiaji 115 walikuwa wanazuiliwa kwenye kambi hiyo iliyoko kwenye jimbo la Saada na inayosimamiwa na Shirika la Kimataifa la Wahamiaji, IOM.