MigogoroUjerumani
Merz: Mazungumzo na viongozi wa Ulaya yamekuwa ya manufaa
13 Agosti 2025Matangazo
Amesema pamoja na mengineyo, viongozi hao wamegusia kwa ufupi kuhusu uhakika wa usalama ambao Ukraine inahitaji.
Aidha Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa aliyeshiriki mazungumzo hayo amesema Rais Donald Trump wa Marekani amesisitiza umuhimu wa Ukraine kushirikishwa kwenye mazungumzo yanayohusiana na maeneo.
Matamshi haya yanaashiria kile kilichofikiwa kwenye mazungumzo hayo baina ya Trump, viongozi wa Ulaya na rais Zelensky yaliyolenga kuchagiza mkutano wa Trump na Rais Vladimir Putin wa Urusi huko Alaska, Marekani siku ya Ijumaa.