Kampuni za China zahimizwa kuheshimu sheria za nchi zilizoko
2 Aprili 2025Matangazo
Siku ya Jumanne jioni, ubalozi huo ulitoa salamu za rambirambi kutokana na kuporomoka kwa jengo hilo na kuzihimiza kampuni zake kuzingatia kikamilifu sheria za Thailand.
Tetemeko la ardhi laporomosha jumba la ghorofa Bangkok
Kwenye chapisho katika ukurasa wa Facebook kwa lugha ya Thai, ubalozi huo umesema serikali ya China, mara kwa mara imezihimiza kampuni zake nje ya nchi kuzingatia sheria za mahali zinakohudumu na kuchangia katika maendeleo chanya ya jamii.
China yatuma wataalmu wa ukoaji Bangkok
Ubalozi huo umeongeza kuwa, serikali yake imetuma timu ya wataalamu wa uokoaji na wafanyakazi wa misaada ya majanga kusaidia katika mkasa huo wa Bangkok na kuahidi kuendelea kuisaidia Thailand kama inavyohitajika.