Matangazo ya sigara zenye ladha yanachochea uraibu Ujerumani
7 Mei 2023Matangazo
Kamishna huyo Burkhard Blienert amesema matangazo ya sigara hizo za kieletroniki zinazotiwa ladha za peremende na matunda yanawachochea vijana kuvuta. Blienert amekosoa kuendelea kwa matangazo ya biashara ya uvutaji wa sigara nchini Ujerumani. Ameliambia shirika moja la habari la Ujerumani, RND kwamba sekta ya tumbaku inatumia Euro milioni 250 kwa ajili ya matangazo ya biashara ya sigara za kiletroniki. Bunge la Ujerumani linatafakari mswaada wa sheria ili kushinikiza hatua ya kupiga marufuku uvutaji wa sigara hizo katika nchi zote za Umoja wa Ulaya.