SiasaSudan
Kambi ya jeshi la anga la Sudan yashambuliwa kwa droni
4 Mei 2025Matangazo
Msemaji huyo ameeleza kuwa mashambulizi hayo yamefanyika kwa kutumia ndege zisizo na rubani, hata hivyo amesema hakuna uharibifu wowote uliotokea. Hayo ni mashambulizi ya kwanza kufanywa na vikosi vya RSF baada ya kuufikia mji huo wa bandari wa mashariki mwa Sudan.
Vikosi vya RSF mpaka sasa bado havijatoa taarifa yoyote kuhusu tukio hilo. Mzozo kati ya jeshi la Sudan na vikosi vya RSF unatajwa na Umoja wa Mataifa kuwa mgogoro mbaya zaidi wa kibinadamu duniani.