SiasaRwanda
Kagame akutana na rais wa zamani wa Nigeria
25 Juni 2025Matangazo
Obasanjo ambaye amekuwa akishiriki katika mchakato wa mazungumzo ya amani katika mzozo wa mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, alijadiliana pia na rais Kagame kuhusu masuala ya kimataifa, ustawi, ushirikiano na maendeleo.
Awali, Ofisi ya rais Kagame mwenye umri wa miaka 67, ilikanusha uvumi kwamba alikuwa mgonjwa kufuatia kutoonekana kwake hadharani tangu Juni 6 mwaka huu.
Mpinzani mmoja anayeishi Canada alidai wiki hii kwamba Kagame alikuwa akisumbuliwa na "tatizo la ubongo" na alikuwa akitibiwa nchini Ujerumani, ingawa chanzo cha kidiplomasia nchini Ujerumani kililiambia shirika la habari la AFP kuwa hawakuwa na taarifa zozote juu ya suala hilo.