Kabila aondolewa kinga ya kutoshitakiwa
23 Mei 2025Matangazo
Kura 88 zilipigwa kuunga mkono hatua hiyo itakayopelekea kiongozi huyo wa zamani kushitakiwa kwa kuwaunga mkono M23.
Spika wa Baraza la Seneti Jean-Michel Sama Lukonde alitangaza baada ya kura hiyo kwamba sasa baraza hilo limeruhusu Kabila kushitakiwa na kuondolewa kinga.
Rais Felix Tshisekedialiyeshika usukani baada ya Kabila, anamtuhumu mtangulizi wake huyo kwa kushirikiana na M23 waliolikamata eneo kubwa la mashariki mwa Kongo.