MigogoroAfrika
SAF na RSF walaumiana kuhusika na shambulio kwenye hospitali
27 Januari 2025Matangazo
Gebreyesus ametoa wito wa kusitishwa kwa mashambulizi yanayolenga vituo vya huduma ya afya na wafanyakazi wake nchini Sudan, akisema kuwa hospitali hiyo ndio pekee inayotoa huduma kwenye mji huo ulioharibiwa na vita.
Soma pia:Watu 70 wauawa katika shambulio la hospitali Sudan
Akielezea shambulio hilo, Gavana wa Darfur Mini Minnawi amesema droni ilishambulia kitengo cha dharura cha hospitali hiyo na kuwauwa wagonjwa wakiwemo wanawake na watoto. Kundi la wapiganaji wa RSF na vikosi vya jeshi la Sudan wametupiana lawama kuhusika na shambulio hilo.