MigogoroUlaya
Jeshi la Russia ladhibiti vijiji viwili katikati mwa Ukraine
26 Julai 2025Matangazo
Mashambulizi ya usiku yaliyofanywa na pande zote mbili yalisababisha vifo vya watu sita, wanne nchini Ukraine na wawili nchini Urusi, kwa mujibu wa maafisa wa nchi zote mbili.
Katika taarifa nyingine Jumamosi, Moscow ilisema imekomboa makaazi ya Zeleny Gai katika eneo la Donetsk, na kuongeza kuwa kilikuwa na kituo muhimu cha ulinzi kilichotumiwa na Ukraine kulinda eneo hilo.
Mashambulizi haya yanaendelea licha ya wito kutoka Marekani wa kusitisha mapigano na kufanyika kwa mazungumzo ya amani huko Istanbul, ambayo hadi sasa hayajazaa matunda.