Jeshi la Israel lasema limemuuwa mratibu wa Iran na Hamas
21 Juni 2025Matangazo
Katika taarifa, jeshi hilo limesema kuwa ndege za kivita za Israelzililenga na kumuuwa kamanda wa Kikosi cha Quds cha Palestina Saeed Izad, ambaye pia ni mratibu mkuu kati ya utawala wa Iran na kundi la kigaidi la Hamas.
Israel yasema bado inaishambulia Iran
Wakati huo huo, jengo la makazi kaskazini mwa Israel limelengwa na droni baada ya jeshi kuripoti kuhusu uvamizi katika bonde la Beit She'an. Haya ni kwa mujibu wa mashuhuda. Aidha, Huduma ya kitaifa ya dharura ya matibabu yaIsraelimethibitisha kuhusu tukio hilo na kuongeza kuwa timu zake za uokoaji hazikupata majeruhi wowote zilipowasili eneo la tukio.