Jeshi la Israel laanzisha operesheni maalum, Lebanon
9 Julai 2025Matangazo
Katika taarifa, jeshi hilo limesema kuwa kufuatia taarifa za kijasusi na pia kutambuliwa kwa silaha za Hezbollah na miundombinu ya kigaidi katika maeneo kadhaa ya kusini mwa Lebanon, wanajeshi walianzisha operesheni maalum, zilizolenga kuzisambaratisha na kulizuia kundi hilo la Hezbollah kujiimarisha tena katika eneo hilo.
Israel kuendeleza mashambulizi dhidi ya Hezbollah
Hata hivyo, jeshi hilo halikujibu mara moja ombi la shirika la habari la AFP la tamko kuhusu iwapo hii ilikuwa mara ya kwanza kwa vikosi vya Israel kutekeleza shughuli zake kwenye ardhi ya Lebanontangu kusitishwa kwa mapigano mnamo mwezi Novemba.