Jeshi la Israel kuwafuta kazi marubani wa akiba
10 Aprili 2025Matangazo
Akizungumzia barua iliyotiwa saini na takriban wanajeshi 1,000 na marubani wastaafu iliyoonekana kwenye vyombo vya habari, afisa huyo ameliambia shirika la habari la Ufaransa AFP kwamba, kwa kuungwa mkono kikamilifu na mkuu wa majeshi, kamanda wa jeshi la anga la Israel, ameamua kuwa wanajeshi wote wa akiba waliotia saini barua hiyo, hawataweza tena kuendelea kuhudumu katika jeshi hilo la Israel.
Wakati huo huo, Wapalestina wapatao 23 wameuawa katika mashambulizi ya Israel yaliyolilenga jengo moja la ghorofa katika Ukanda wa Gaza.