JD Vance azitaka Urusi na Ukraine kufikia makubaliano
23 Aprili 2025Matangazo
Onyo la kiongozi huyo wa Marekani amelitowa wakati ukifanyika mkutano unaowakutanisha wajumbe wa Marekani, Ukraine na Umoja wa Ulaya nchini Uingereza wa kujaribu kushinikiza kumalizika kwa vita vya Ukraine.Soma pia: JD Vance akutana na Narendra Modi mjini New Delhi
Vance amewaambia waandishi habari akiwa kwenye ziara ya siku nne nchini India, kwamba Marekani imetowa pendekezo maalum kwa pande zote mbili, Urusi na Ukraine, na zinapaswa ama kukubaliana na pendekezo hilo au Marekani itajiondowa kwenye mchakato wa kutafuta amani.Soma pia : Mkutano wa ngazi ya juu kuhusu Ukraine wagonga mwamba