JangaJapan
Japan yapambana na moto mkubwa wa nyika kuwahi kushuhudiwa
1 Machi 2025Matangazo
Mtu mmoja ameripotiwa kufariki huku mamia ya wengine wamehamishwa. Shirika la Kudhibiti Majanga la Japan limesema takriban maafisa wa zimamoto wapatao 1,700 wamekusanywa kote nchini ili kukabiliana na moto huo ulioanza siku ya Jumatano.
Inaaminika moto huo umesambaa katika eneo lenye ukubwa wa ekari 3,000 katika msitu waOfunato katika mkoa wa kaskazini wa Iwate. Mamlaka za Japan zimesema moto huo wa nyika ni mkubwa zaidi kuliko ule uliotokea mwaka 1992 huko Kushiro kisiwani Hokkaido ambao uliteketeza hekta 1,030.