Jamii ya LGBTQ inaishi kwa hofu, Uganda
26 Mei 2025Matangazo
Shirika hilo liliwahoji watu takriban 60 wa Jamii hiyo, familia zao, wanaharakati na wanasiasa kuandaa ripoti ya athari ya sheria hiyo iliyopitishwa mwaka 2023.
Sheria hiyo iliweka adhabu ya kifungo cha maisha kwa wanaoshiriki vitendo hivyo na hata kutoa adhabu ya kuuwawa kwa watakaopatikana na hatia ya kushiriki mapenzi ya jinsia moja.
Mahakama Uganda yatupilia mbali shauri la kupinga sheria dhidi ya LGBTQ
Oyem Nyeko moja ya watafiti katika shirika la Human Rights Watch ameliambia shirika la habari la AFP kwamba mashoga na wasagaji nchini Uganda wanaishi kwa hofu kwa sababu kuna sheria zinazohalalisha watu kuwafanyia vitendo vya vurugu dhidi yao.